24 Februari 2026 - 10:03
Source: ABNA
Tamko la Nchi 20 za Kiislamu na za Kizungu Kulaani Utawala wa Israel Ukingoni mwa Mto Jordan

Nchi ishirini za Kiarabu, Kiislamu na za Kizungu zimekulaani utawala wa Israel ukingoni mwa Mto Jordan.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Mehr lenye kunukuu kutoka kwenye mtandao wa Al Jazeera, nchi 20 zikiwemo za Kiislamu, Kiarabu na za Kizungu zimetoa tamko la pamoja, na kulaani vikali maamuzi ya Israel ya kupanua udhibiti wake haramu ukingoni mwa Mto Jordan.

Katika tamko hili imesisitizwa kuwa makazi ya Israel ni kinyume cha sheria na upanuzi wake ni ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa.

Waliotia sahihi katika tamko hili pia walitangaza kwamba maamuzi ya hivi karibuni ya Israel yamechukuliwa kwa lengo la kuelekea kwenye kuiunganisha ng'ambo ukingoni mwa Mto Jordan na maeneo mengine yanayokaliwa kwa njia isiyokubalika.

Tamko hili linaongeza kuwa hatua za Israel kuelekea ukingoni mwa Mto Jordan zinadhoofisha juhudi za kufikisha amani katika eneo hili, pamoja na mipango inayohusiana na Gaza, na itakuwa na matokeo mabaya kwa utulivu wa eneo zima.

Nchi zilizotajwa pia ziliiomba Israel kujiondoa kwenye maamuzi yake kuhusu ukingoni mwa Mto Jordan.

Katika tamko hili imesisitizwa: Tunaiomba Israel ikomeshe vurugu za walowezi na kuwatoa hatiani wale wanaokiuka sheria (ya kukomesha vurugu dhidi ya watu wa Palestina).

Nchi 20 zilizotajwa hapo juu pia zilitangaza upinzani wao mkali dhidi ya kubadilisha muundo wa idadi ya watu na hali za ardhi toka mwaka 1967 ikiwemo katika Jerusalem ya Mashariki.

Your Comment

You are replying to: .
captcha